Thursday 5 January 2017

Mpunga ni zao ambalo hupendwa na watu wengi sana hususani katika bara la Afrika na ni zao la pili kwa uzalishwa kwa wingi sana. Kilimo hiki cha mpunga ni zao la chakula na la biashara.Kilimo hiki hushamiri zaidi katika maeneo yenye maji mengi na mvua ya kutosha.
Kuna mbegu mbalimbali ambazo wakulima wengi huzitumia kama vile; 
NJIA YA KUTIBU MBEGU KABLA YA KUPANDA SHAMBANI
Kuna njia kuu tatu 
(I) Ni kusafisha mbegu kwa kutumia maji ya uvuguvugu,chukua maji yako uliyopasha moto, weka mbegu zako katika mfuko wa pamba na ingiza mbegu zako ndani ya maji hayo ya uvuguvugu. Baada ya kufanya hivo Toa mbegu zako kwenye mfuko na zianike katika karatasi kavu ili zipoe na kukauka.Kwa kutumia njia inasaidia kuondoa wadudu waliomo ndani ya mbegu. 
(ii) Kuloweka mbegu,hii inafanya mbegu ipate unyevunyevu wa kutosha kuchipua,pia kuzuia mbegu kuoza. Wakati wa kuloweka badilisha maji ili kuondoa viini venye simu.
(iii) Kabla ya kuchipua,kausha mbegu na zifunike na jamani kwa masaa 24 had I 48. Inasaidia kuhakikisha kuwa mbegu zinachipua kwa wakati mmoja.
HATUA ZA KUTAYARISHA SHAMBA LA MPUNGA
-Itakuwa vizuri zaidi kulima shamba angalau siku 15 kabla ya kupanda niche au mbegu moja kwa moja. Inasaidia kulinda niche isiharibiwe na wadudu na kuzuia kupotea kwa nitrogeni.
-Matayarisho ya shamba kwa kulima Aisha kwa mkono au ng’ombe au trekta baada ya mvua kunyesha.
-Hatua inayofuata ni kulainisha udongo kwa kupiga piga ili use uji au vipande kidogo.
-Kitendo kinachofuata ni kupanda niche shambani,lakini katika hatua hii kuna wengine huwa haaa wanapanda mbegu moja kwa moja.
Hatua ya palizi ya kwanza na ya pili hufanyaka,lazima kung’oa magugu au kupiga sawa ya viua gugu.
-Pia mbolea za kupandia na kukuzia huhusika baada ya kupandikiza miche shambani na matumizi ya dawa za wadudu pia hutumika kama kuna uhitaji.
-Unashauriwa kuvuna kwa kukata masuke,kupiga masuke kupata mpunga.
NJIA ZA KUPANDIKIZA MBEGU
kuna njia mbili ambazo wakulima hutumia kupanda mbegu za MPUNGA shambani
(i) Kuondoa miche kwenye kitabu na kuipanda shambani Mara tu inapofikia hatua ya kupanda. Niche hii itakuwa tayari kati ya wiki tatu hadi nne tangu kuotesha.
(ii) Kupanda mbegu moja kwa mojanjia hii inatumiwa na wakulima wengi kwa muda mrefu ambapo mbegu za MPUNGA hutawanywa shambani moja kwa moja.Hivyo njia husababisha uzalishaji kupungua na shamba kuwa magugu mengi.
WADUDU WAHARIBIFU KWENYE KILIMO CHA MPUNGA 
Uharibifu wa mpunga hutokana na vijidudu,mimea au wadudu ambayo wanauwezo wa kushusha kiwango cha uzalishaji wa mmea. Wapo wadudu wengi sana wanaoathiri mpunga katika ukuaji wa hatua mbalimbali.Wadudu hao ni kama, mafunzo (stemborers),African rice gall midgeAFRGM, na Orseolia oryzyvora. Wadudu hawa wamekuwa tishio sana katika zako hili la MPUNGA.
UVUNAJI
MPUNGA kuchukua Kati ya miezi minne (4) hadi sita (6) kutokana na aina ya mbegu uliyotumia baada ya kupanda mpaka wakati wa kukomaa.

0 comments:

Post a Comment

TANGAZA NASI KWA BEI NAFUU

TANGAZA HAPA

Powered by Blogger.

TANGAZO TANGAZO

TUNATENGEZA MACHINE ZA INCUBATOR KWA BEI POA.
HII NI OFA KWA AJILI YA MWAKA MPYA 2018. KARIBUNI SANA.

Video

Popular Posts

Our Facebook Page